Mchungaji Matumika amelala usingizi wa mauti tarehe 14/07/2012 na mazishi yake yamefanyika tarehe 17/07/2012 jijini Mbeya.

 

HISTORIA FUPI YA MCHUNGAJI HAMISI EMMANUEL MATUMIKA

KUZALIWA

Alizaliwa mwaka 1942 kule North Pare

Alioa    31/12/1967

UTUMISHI

Aliajiriwa na Kanisa mwaka 1966 kama Mhasibu, South Nyanza Field

Elimu alienda Bugema College 1968. Alirudi mwaka 1969  na kuwa Mhasibu South Nyanza Field

Alikuwa Katibu na  Mhazini Msaidizi wa Central Nyanza Field 1971 – 1972

Mwaka 1973 alikuwa Mchungaji wa Mtaa   - Songea

Mwaka 1985 alienda Chuoni Arusha Seminary

Mwaka 1986 alikuwa Mchungaji  wa  Mtaa –Njombe

Mwaka 1993 Alikuwa Mkurugenzi   wa Huduma

Mwaka 1996 - 2003 Mchungaji wa Mtaa- Njombe

Mwaka 2004 – 2005 alikuwa Mchungaji wa Mtaa Mbalizi  na mnamo January 2006 alipumzika kazi ya kuongoza Mtaa (alistaafu kazi)

MAGONJWA

Mnamo mwaka  2003 alipata ugonjwa wa Kisukari  ambacho kimekuwa kinamsumbua mara kwa mara.

MAUTI

Tarehe 10/7/2012 alianza kuumwa  tarehe 13/7/2012 alipelekwa Hospitali ya  Mkoa.  Tarehe 14/7/2012 asubuhi mnamo saa 3 alilala mauti.

 

 
Adventist News Network
Southern Highlands Conference